Kesi ya Hamad yasomwa, CUF wapiga chenga
Mbunge wa Wawi Hamad Rashid Mohamed, ameitaka Mahakama kutoa amri kwa Wadhamini wa chama cha Wananchi CUF kuja mahakamani, baada ya wahusika wa chama hicho kutotokea kusikiliza kesi hiyo iliyolenga kukisulubu kwa kumfukuza yeye uanachama na wenzake 10. 

Katika kesi hiyo nambari 1 ya mwaka 2012, mbunge huyo pamoja na wenzake hao wanaitaka Mahakama kuamuru chama hicho cha wananchi kubatilisha mara moja uamuzi wa viongozi wake kuwafukuza uanachama wakidai kuwa wao ni wanachama halali kikatiba.
Mahakama kuu ilipanga kusikiliza kesi hiyo rasmi hii leo, kujiridhisha na ushahidi wa madai yaliyowasilishwa hapo na walalamikaji, dhidi ya chama cha CUF.
Top Stories »





