Home | Dar-es-Salaam weather Partly Cloudy and 25 C Dar-es-Salaam weather
RSS News
Entertainment

In this section you can find out the latest news
and gossip in Bongo, the hottest music videos from
your favorite artists and from a few up and coming acts,
what celebrities got up to while they were at school,
the latest street words, and what's happening in your
favorite soap opera.

Entertainment

Fataki zapigwa marufuku sikukuu kesho
Wakati Jumuiya ya Kiislamu nchini ikijiandaa kwa sikukuu ya Eid El Fitri kesho Ijumaa baada ya mwezi kuandama jioni hii, shambrashambra za kusheherekea siku hiyo kwa kupiga fataki juu zimepigwa marufuku huku Jeshi la Polisi likitoa angalizo kwa suala zima la usalama.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova, katazo hilo limetolewa kuepusha rapsha zozote zinazoweza kutokea kutokana na milipuko ya fataki hizo.

Kadhalika Kamanda Kova amewataka wazazi wote kuhakikisha usalama wa watoto wao kwa kutowaacha kutembea njiani bila uangalizi na kuonya juu ya kutoka majumbani na kuacha bila ulinzi thabiti kuepusha wizi unaoepukika.

Aidha mkuu huyo wa polisi amewaonya madereva wa daladala kote jijini katika kubeba abiria kupita kiasi pamoja na kuepuka kutumia magari ya wazi kama Canter na Malori kubebea abiria.

Reviews


Comment Preview

Live Music

This text will be replaced by the flash music player.