Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM sawa na Kaimu Mwenyekiti wa Chama hicho Pius Msekwa, wameunga mkono hatua ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU, kuwakamata baadhi ya makada wao wa chama hicho kwa kutuhumiwa kuhusika na masuala ya rushwa.
Akizungumzia suala hilo jijini Dar es Salaam leo, Makamba amesema mwanachama wa chama hicho atakayethibitika kuhusika na suala la rushwa hatatetewa kwa kuwa ni kinyume na utaratibu na pia katiba ya chama inakataza.
‘kama mtu atashikwa, TAKUKURU endelea naye’ amefafanua Makamba
Naye Kaimu mwenyekiti wa Chama hicho Pius Msekwa amesema rushwa ni kosa la jinai kama yalivyo makosa mengine kama ya wizi au mauaji, na kwamba sheria inapaswa kutenda inavyotakiwa.
Remember my personal informationNotify me of follow-up comments?
Submit the word you see below: