<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<rss version="2.0"
    xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
    xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
    xmlns:admin="http://webns.net/mvcb/"
    xmlns:rdf="http://www.w3.org/1999/02/22-rdf-syntax-ns#"
    xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/">

    <channel>
    
    <title>Entertainment</title>
    <link>http://www.dar411.com/index.php?/entertainment/</link>
    <description></description>
    <dc:language>en</dc:language>
    <dc:creator>jushaj@dar411.com</dc:creator>
    <dc:rights>Copyright 2010</dc:rights>
    <dc:date>2010-09-09T17:18:00+03:00</dc:date>
    <admin:generatorAgent rdf:resource="expressionengine" />
    

    <item>
      <title>Fataki zapigwa marufuku sikukuu kesho</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/fataki_zapigwa_marufuku_sikukuu_kesho/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/fataki_zapigwa_marufuku_sikukuu_kesho/#When:17:18:00Z</guid>
      <description>Wakati Jumuiya ya Kiislamu nchini ikijiandaa kwa sikukuu ya Eid El Fitri kesho Ijumaa baada ya mwezi kuandama jioni hii, shambrashambra za kusheherekea siku hiyo kwa kupiga fataki juu zimepigwa marufuku huku Jeshi la Polisi likitoa angalizo kwa suala zima la usalama.Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova, katazo hilo limetolewa kuepusha rapsha zozote zinazoweza kutokea kutokana na milipuko ya fataki hizo.


Kadhalika Kamanda Kova amewataka wazazi wote kuhakikisha usalama wa watoto wao kwa kutowaacha kutembea njiani bila uangalizi na kuonya juu ya kutoka majumbani na kuacha bila ulinzi thabiti kuepusha wizi unaoepukika.


Aidha mkuu huyo wa polisi amewaonya madereva wa daladala kote jijini katika kubeba abiria kupita kiasi pamoja na kuepuka kutumia magari ya wazi kama Canter na Malori kubebea abiria.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-09T17:18:00+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Yanga yawanyuka Wakenya</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/yanga_yawanyuka_wakenya/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/yanga_yawanyuka_wakenya/#When:18:07:01Z</guid>
      <description>Timu ya soka ya Yanga kutoka Dar es Salaam, imefanikiwa kuibuka kidedea katika mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Klabu ya soka kutoka Kenya AFC Leopard, baada ya kuwanyuka kwa bao 1 bila majibu katika kiwanja  cha Sheikh Amri Abeid cha mjini Arusha yalipo makazi ya Klabu ya soka ya AFC ya mjini Arusha.Akizungumza baada ya mchuano huo mkali baina ya vinara hao wawili, Kocha Mkuu wa Klabu ya AFC Leopard kutoka Kenya Dino Kitavi amesema timu ya Dar Young Africans imestahili ushindi kutokana na uzoefu wake kisoka, na kuongeza kuwa mchezo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili.


Wakati huo huo kitendawili kimezidi kutawala juu ya uwanja gani Yanga itumie kwa michezo yake ya nyumbani, baada ya Serikali kusuasua kutoa majibu juu ya ombi lao la kuutaka uwanja wa Taifa , hivyo kulazimika pia kujiandaa kutumia kiwanja cha Jamhuri mjini Morogoro kama ombi hilo litatupiliwa mbali.

hata hivyo kwa taarifa hazijathibitishwa zilizotufikia hivi karibuni, zinasema tayari Wanajangwani hao Yanga wamesharuhusiwa kutumia kiwanja hicho cha Jamhuri mjini Morogoro.</description>
      <dc:subject>Sports News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-08T18:07:01+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Utata kiwanda cha Mtibwa Morogoro wazimwa</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/utata_kiwanda_cha_mtibwa_morogoro_wazimwa/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/utata_kiwanda_cha_mtibwa_morogoro_wazimwa/#When:17:48:00Z</guid>
      <description>Sakata la malumbano na kutoelewana baina ya Wamiliki na Wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari cha mkoani Morogoro, umepatiwa ufumbuzi baada ya kauli ya Raisi Kikwete iliyowataka wahusika kufanya mkutano wa kumaliza mvutano mara moja.Akizungumza baada ya mkutano huo uliofanyika kuihusisha Menejimenti ya Kiwanda hicho pamoja na Wafanyakazi katika mashamba ya miwa pamoja na wale wa kiwandani, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Bi Fatma Mwasa amesema changamoto kuu zilizokuwa zimesababisha mvutano zimezungumzwa na kutatuliwa hivyo kurejesha hali ya ustawi katika sekta hiyo.


Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na malalamiko ya Wafanyakazi wadogowadogo wa mashamba ya miwa pamoja na wale wa viwandani kudai kupata lugha chafu na za vitisho kutoka kwa mmiliki wa kiwanda hicho, kutokuwepo kwa mkataba maalumu wa kufanya kazi, ucheleweshwaji wa malipo ya pensheni pamoja na changamoto nyingine zinazofikia 10, ambapo Bi Mwasa amesema yote yametatuliwa.


Ufumbuzi huo umekuja baada ya Raisi Kikwete kupata malalamiko hayo alipokuwa katika harakati za kampeni, na kuagiza ufumbuzi utafutwe mapema ambapo aliahidi kurejea tena kiwandani hapo kuona kama matatizo yamekwisha au la. 


Kadhalika miongoni mwa maamuzi na maafikiano yaliyofikiwa ni pamoja na kufukuzwa kwa Meneja mkuu wa Kiwanda hicho kutoka Afrika ya Kusini aliyetajwa kwa jina moja la Grayson, na kwamba pamoja na kufukuzwa kazi, pia ameamrishwa kuondoka nchini, akituhumiwa  kutumia lugha ya matusi kwa wafanyakazi na kutowajali.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-08T17:48:00+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Uzalishaji wa sumu sasa kudhibitiwa Dar</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/uzalishaji_wa_sumu_sasa_kudhibitiwa_dar/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/uzalishaji_wa_sumu_sasa_kudhibitiwa_dar/#When:17:03:00Z</guid>
      <description>Asasi mbalimbali za kuhifadhi mazingira kwa kushirikiana na Shirika la viwango nchini TBS, leo wamekubaliana kupitisha rasimu ya viwango vya mabaki yanayotakiwa kuingizwa katika mazingira, kwa lengo la kuepusha uchafuzi wa mazingira yetu.Akizungumza katika mkutano wa pamoja wa wadau hao wa mazingira, maofisa wa TBS pamoja na asasi mbalimbali nchini, Afisa Mkuu wa viwango wa TBS Leandry Kinabo amesema sumu zilizolengwa katika rasimu hiyo ni maji machafu yenye sumu kutoka viwandani yanayoelekezwa ardhini na baharini, hewa chafu ya viwandani (moshi wa sumu), pamoja na taka ngumu zinazotupwa ovyo juu ya uso wa ardhi na majini.


Amesema Rasimu hiyo imepitishwa na Wadau wote na kwamba sasa itapelekwa kwa wahusika mbalimbali wa mazingira pamoja na wale wanaozalisha taka hizo, ili kutoa maoni yao juu mapendekezo na hatua za rasimu hiyo na hatimaye katika kipindi cha miezi sita ijayo kutoka sasa, itapitishwa rasmi kuwa sheria ya kulinda mazingira yetu. 


Rasimu hiyo inajadiliwa hivi sasa katika wakati ambao jiji la Dar es Salaam linazidi kukua huku viwanda vikizidi kuongezeka pamoja na shughuli mbalimbali za kibinadamu zinazoonyesha kuchafua mazingira, hivyo kupitishwa kwa rasimu hiyo kutaweza kuondoa hatari ya jiji kugeuka dampo na mahali pasipofaa kuishi binadamu na viumbe vingine hai.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-08T17:03:00+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Prof Jay: akana kukutana na Bill Gates</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/prof_jay_akana_kukutana_na_bill_gates/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/prof_jay_akana_kukutana_na_bill_gates/#When:07:21:00Z</guid>
      <description>Hivi Karibuni zilitapakaa Habari kwenye mitandao ya Internet kuwa Msanii wa Hip Hop Prof Jay amekutana na tajiri mwenye mkwanja mrefu duniani Bill Gates katika ofisi zake na kuongea mawili matatu. Hivi Karibuni zilitapakaa Habari kwenye mitandao ya Internet kuwa Msanii wa Hip Hop Prof Jay amekutana na tajiri mwenye mkwanja mrefu duniani Bill Gates katika ofisi zake na kuongea mawili matatu. Prof Jay amezikanusha habari hizo na kusema SI ZA KWELI lakini yeye alitembelea Office zake tu na wala si kukutana na Bill Gates</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-08T07:21:00+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Alikiba Ajitoa Records</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/alikiba_ajitoa_records/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/alikiba_ajitoa_records/#When:06:50:00Z</guid>
      <description>baada ya kufanya kazi na G Records, kwa Takribani miaka kadhaa tangu utambulisho katika industry ya Bongo Fleva msanii wa kizazi kipya Ali kiba ameamua kuachana na uongozi huo na kuamua kufanya kazi zake mwenyewe.baada ya kufanya kazi na G Records, kwa Takribani miaka kadhaa tangu utambulisho katika industry ya Bongo Fleva msanii wa kizazi kipya Ali kiba ameamua kuachana na uongozi huo na kuamua kufanya kazi zake mwenyewe.

C.E.O wa G records Guru Ramadhan ameongeza kuwa Kwa sasa wamebaki na album mbili baada ya Alikiba kuomba kufanya kazi zake mwenyewe.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-08T06:50:00+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Godzilla: Kuzindua Godzilla Inc</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/godzilla_kuzindua_godzilla_inc/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/godzilla_kuzindua_godzilla_inc/#When:21:33:03Z</guid>
      <description>Msanii wa bongo fleva anayejulikana kwa jina la Godzilla King of Salasala ameanzisha lebo yake inayokwenda kwa jina la Godzilla Inc!
GodZilla amesema lebo hiyo itakuwa ikiwasupport wasanii undergrounds wanao chana lakini hawajapata nafasi ya kuingia studioMsanii wa bongo fleva anayejulikana kwa jina la Godzilla King of Salasala ameanzisha lebo yake inayokwenda kwa jina la Godzilla Inc!

GodZilla amesema lebo hiyo itakuwa ikiwasupport wasanii undergrounds wanao chana lakini hawajapata nafasi ya kuingia studio. Godzilla ameongeza kuwa Label yake itakua tayari kukusaidia endapo una uwezo na unahitaji msaada.Dar411 inakutakia mafanikio mema Godzilla kwa ulichopanga kufanya.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-07T21:33:03+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Ben Pol = Msanii anayekuja kwa kasi</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/ben_pol_msanii_anayekuja_kwa_kasi/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/ben_pol_msanii_anayekuja_kwa_kasi/#When:20:24:02Z</guid>
      <description>Ni msanii anayekuja kwa kasi na ni mmoja wa vijana aliye chini ya usimamizi wa Duke Tachez kutoka M lab studio ambayo iko chini ya Duke. Jina lake Halisi ni Benard Paul mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, lakini kwa jina la kisanii anajulikana zaidi kama Ben Pol.
Ben Pol alianza kujigundua kuwa ana kipaji cha muziki akiwa Darasa la Tano ambapo nyimbo yake ya kwanza aliandikiwa na Baba yake mdogo hiyo ilikua mwaka 2001. na akaachana na mambo ya muziki na kufanya sanaa za shule zaidi ikiwa na kuigiza na mambo mengine.Ni msanii anayekuja kwa kasi na ni mmoja wa vijana aliye chini ya usimamizi wa Duke Tachez kutoka M lab studio ambayo iko chini ya Duke. Jina lake Halisi ni Benard Paul mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, lakini kwa jina la kisanii anajulikana zaidi kama Ben Pol.

Ben Pol alianza kujigundua kuwa ana kipaji cha muziki akiwa Darasa la Tano ambapo nyimbo yake ya kwanza aliandikiwa na Baba yake mdogo hiyo ilikua mwaka 2001. na akaachana na mambo ya muziki na kufanya sanaa za shule zaidi ikiwa na kuigiza na mambo mengine.

Kufikia Form two Ben Pol alikutana na Msanii mwenzake ambaye kwa sasa wako label moja anayejulikana kama Stereo. Hii ilitokana na kuwa msiri kwa mambo yake. Na kwa mara ya kwanza aliandika Verse yake mwenyewe na stereo kugundua kuwa ana style nzuri ambayo ingeweza kumuweka juu kimuziki na stereo kumtambulisha kwenye studio ya kaka yake iliyokua ikiitwa Big Boys producer akiwa ni Prof Ludigo.


Siku ya kwanza kuingia studio hapo hawakufanikiwa kurecord kwa sababu ya umeme kukatika. Wakiwa kwenye harakati ya kutafuta kutoka kimuziki, Waliingia kwenye Tamasha la WAPI na walifanikiwa kukutana na watu kama Joh Makini, Fid Q na wengine kibao. na mtu aliyemshawishi zaidi ukiacha stereo, Ni kama Prof Jay ambaye kwa kipindi iko na mpaka sasa ni mtu ambaye alikua akwepeki kukufanya uwe unampenda na Ben Pol kutamani kuwa mwanamuziki. Kufikia Form 4 mwaka 2006 &#45; 2007 alifanikiwa kutoa nyimbo ambayo ilikua inaitwa nikupendae ambayo ilikua na Mistari minne tu. ambayo ilikua ijijirudia na baada ya kumuonesha stereo alimshauri kuanza kuimba na si kurap. Na stereo alipata wazo la kumshauri kuacha kurap na aanze kuimba kama wasanii wengine kama Barnaba, Amini na wengineo.


Ben Pol hakuweza kujikita zaidi kwenye zaidi kwenye muziki kwa kipindi icho kutokana na shule na kuona wakati utafika na atakuja kuanza kufanya Rasmi. Mwaka 2009 Ben Pol  kwa mara ya kwanza aliitwa Mlab kuingiza Hard Lips kwenye wimbo wa Musa vipaji vingi ambao wimbo huo Ben pol alishiriki kuandika maneno ya Kigogo. 

Baada ya kumaliza ya kumaliza Shule 2010, Ben Pol alifanikiwa kuingia mkataba na M lab hii ilitokana baada ya producer Duke kujua kipaji cha Ben Pol na kuona wanaweza kufanya pamoja na Siku ambayo Duke alimkubali zaidi Ben Pol siku ambayo Nikki Mbishi alikua akifanya track yake ya Play Boy na Ben Pol alipita Studio kusalimia na bahati nzuri alifanikiwa na kuombwa kufanya Part ya kiitikio cha Play Boy. Kiukweli Ben Pol alifanya vizuri katika kiitikio hicho na kuzidi kumshawishi Duke kumuhitaji zaidi kufanya nae kazi. na Duke alimuhita kwa mara ya mwisho na kumfanyia majaribio ya mwisho ambayo alipewa beat ambayo aliyotakiwa kuandikia na Ben Pol kwa mara ya kwanza alifanikiwa kurecord track yake iliyokwenda kwa jina la PATA RAHA (SIKILIZA KWENYE PLAYLIST) ambayo aliandika akiwa studio na alifanikiwa kuwashirikisha wasanii wenzake ambao ni Stereo, One na nikki mbishi.


Ben Pol safari yake ya kimuziki ikaanzia hapo na wimbo kuanza kupigwa katika vituo mbali mbali vya Radio na Ben Pol akaingia mkataba rasmi na M lab wa kufanya kazi zake za kimuziki. na kufanikiwa Kurecord nyimbo ya pili ambayo  ilikwenda kwa jina la NIKIKUPATA amabayo iko Radio na inazidiki kufanya Vizuri (SIKILIZA KWENYE PLAYLIST) Ben Pol akuishia Hapo ameshawahi shirikishwa katika nyimbo kadhaa kama Play Boy ya Nikki Mbishi na My Time ambayo amehirikishwa na Nendeze, Angeris, baby Jay, Pipi, Linah, Mary Lucas, Aneth, Chiku K &amp;amp; Vanessa. hii ni Nyimbo ambayo imetoka Hivi karibuni ikiwa imefanywa M lab na Producer Duke ambaye anafanya Mixtape ya New Era Muzik. 

Ben Pol kwa sasa yuko mbioni kutoa video yake ya nikikupata ambayo amefanya na Adam Juma wa visual Lab ambayo itatoka hivi karibu. na yuko mbioni kutoa album ambayo bado hajaipa jina na iko jikoni na soon itatangazwa jina.

Ben Pol anatoa shukrani kwa Wazazi wake kwa kumpa moyo, mashabiki wake kwa kumsapoti katika shughuli zake za kimuziki na kupokea kazi zake vizuri, Producer Mbezi, THT, Musa Vipaji Vingi, Stereo, na management nzima ya Mlab na wengine Wengi ambao kwa namna yoyote wamefanikiwa kumsaidia katika shuguli zake za kimuziki.

Huyu ndiye Ben Pol.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-07T20:24:02+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Zanzibar wamchefua kocha mpya</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/zanzibar_wamchefua_kocha_mpya/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/zanzibar_wamchefua_kocha_mpya/#When:17:30:02Z</guid>
      <description>Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Zanzibar Mwingereza Stewart John Hall ameondoka kwa hasira katika kiwanja cha mazoezi cha Amani mjini Zanzibar, baada ya kutakiwa kutofanya mazoezi kwenye eneo hilo na wamiliki wa kiwanja hicho.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Mpira la Zanzibar ZFA Maulid Hamad Maulid, ni kweli kocha huyo amekasirishwa na hatua hiyo na kusema kuwa kuna tofauti katika ya Shirikisho la Mpira na serikali katika umiliki wa kiwanja, hivyo kueleza ZFA haiwezi kuidhinisha kutumika kwa kiwanja hicho kwa kuwa hakiko chini yake.


Afisa huyo amesema Mazoezi ya timu hiyo ya Taifa katika kiwanja cha Amani yasingechukua muda zaidi siku moja, kwa kuwa watakwenda kwenye mechi za majaribio nje ya Zanzibar.


Hata hivyo mazoezi ya timu hiyo ya Taifa ya Zanzibar maarufu kama Zanzibar Heroes yameendelea chini ya Kocha huyo katika kiwanja kingine cha Mao Zeitung huko huko Zanzibar.</description>
      <dc:subject>Sports News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-07T17:30:02+03:00</dc:date>
    </item>

    <item>
      <title>Pingamizi la Kikwete, CHADEMA kutoenda Mahakamani</title>
      <link>http://www.dar411.com/index.php?/site/pingamizi_la_kikwete_chadema_kutoenda_mahakamani/</link>
      <guid>http://www.dar411.com/index.php?/site/pingamizi_la_kikwete_chadema_kutoenda_mahakamani/#When:16:44:00Z</guid>
      <description>. Tendwa asisitiza uamuzi wake kufuta pingamizi hilo ni sahihi
. Wananchi waaswa kupima uhalali wa maamuzi hayo ya tume
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo nchini CHADEMA, kimejibu uamuzi wa Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa kuwa si madhubuti haukutenda haki na haukuzingatia kiini halisi cha pingamizi lenyewe, na kusisitiza kuwa  bado wanahitaji haki itendeke.
Akizungumza na Wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Mwanasheria mkuu wa Chama hicho Mabere Marando amesema ni maamuzi yasiyo na haki yaliyoshindwa kuzingatia uzito wa jambo hilo na kueleza Msajili alijiundia utaratibu wake kinyume na sheria katika suala hilo, na kwamba sheria ya uchaguzi imekiukwa waziwazi kwenye shauri hilo.


Wakati huo huo, Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji John Tendwa, amesisitiza kuwa uamuzi wake juu ya kutupilia mbali shitaka hilo la CHADEMA ni sahihi, na kwamba iwapo hawajaridhishwa na uamuzi huo wakate rufaa na kwenda Mahakamani.


Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni wa Chama Cha CHADEMA Prof. Mwesiga Baregu amewataka Wananchi wa Tanzania kupima wenyewe hukumu ya  pingamizi hilo, kwa kuona ni kwa jinsi gani haki inavyokanyagwa na kushauri kuwa waamue katika kura zao, kukomboa Taifa hili na mustakabali wa maisha yao ya baadaye, kwa kuwa ndiyo njia pekee inayoweza kutumika kujikomboa.</description>
      <dc:subject>Entertainment News</dc:subject>
      <dc:date>2010-09-07T16:44:00+03:00</dc:date>
    </item>

    
    </channel>
</rss>